Kifo cha mtoto Baranyikwa Dismas
Bwana alitowa na bwana ametwa ,Jina la Bwana litukuzwe. Amin
Ni katika hali ya masikitiko makuba sana tulipo pata taarifa za kifo cha Shujaa mototo Baranyikwa Dismas ambae kwa kipindi cha miaka kumi na sita hivi alikuwa akisumbuliwa na gonjwa hatari la ukimwi…Na kwa bahati mbaya sana kwa kipindi kirefu hakutambul;ika nini iilicho kuwa kina msibu hadi hivi karibuni ilipogundulika kwamba laizaliwa na Vijidudu vinavyo sababisha ugonjwa wa ukimwi. Hakuna na kosa lolote lile kwa ameenda kwa baba yetu alie mbinguni akiwa safi kutokana na umri wake na kuzaliwa akiwa tayari ameathirika. Shujaa wetu huyo hakusita katu kuudhurishia ulimwengu na ndugu na jamaa wote kwamba tayari anasumbuliwa na gonjwa hilo hatari , na kutokana na msaada wa mara kwa mara kutoka kwa Ndugu Noe SEBISABA ambaye kwa kipindi irefu alikuwa mlezi wake na ndugu wa karibu , Baranyikwa aliweza kuishi katika ulimwengu huu bila majonzi makubwa ukilinganiosha na hali halisi ya afya yake kama mwenyewe alivyo sema ” Toka nilipojitangaza kwamba mimi ni mgonjwa wa ukimwi, nilipata nafuu sana na hata mwili wangu na uzito umeongezeka , hapo zamani nilikuwa kama nyasi ”
Tunatowa shukrani kwa wale wote kwa mabli ama kwa karibu waliweza kuwa na kijana wetu huu katika kipindi kigumu cha maisha yake hapa Duniani, na shukrani za dhati sana kwa ndugu Noe SEBISABA kwa moyo wa ukarimu uliyouonesha kwa kipindi chote hichi. Na hatiamye ni kwa jamii ya kitaifa na ile ya kimataifa kutupia jicho kwa wale ndugu zetu ambao kwa sababu mbali mbali zikiwemo za umasikini ama kutokuelewa ama maisha wamejikuta tayari wameambukizwa, kutowa msaada hususan kwa wale mayatima wa janga hili.